Powered By Blogger

Tuesday 9 October 2012

Alice Were for County/Consituency leadership | Home Page

Alice Were for County/Consituency leadership | Home Page

Friday 5 October 2012

Spidery black objects on Mars surface raise speculation

Someone alert Ziggy Stardust, there appear to be spiders on Mars.

Strange black objects seen from 200 miles above the surface of Mars are generating interest and speculation that the unidentified objects could be anything from geysers to sunbathing colonies of microorganisms.

NPR presents several photos of the objects, including one taken by the Mars Reconnaissance Orbiter on Jan. 27, 2010, that appears to show "little black flecks dotting the ridges, mostly on the sunny side, like sunbathing spiders sitting in rows."

The objects were first spotted in 1998. Interestingly, they appear when the surface of Mars begins to warm, showing up in the same location most of the time. And then when the Martian winter approaches, they disappear with the same precise regularity. The images have been brought into greater detail by Michael Benson in his book "Planetfall: New Solar System Visions."

Most scientists, including teams from the U.S. Geological Survey, Hungary and the European Space Agency, have their own theories, but the leading explanation is that the objects are geysers of CO2 exploding from underneath the planet's surface.

"If you were there, you'd be standing on a slab of carbon dioxide ice," Phil Christensen of Arizona State University told NPR. "All around you, roaring jets of carbon dioxide gas are throwing sand and dust a couple hundred feet into the air. The ground below would be rumbling. You'd feel it in your space boots."

And while the geyser theory is the most popular explanation, it has yet to be verified.

In the meantime, there are some interesting alternative theories, including one from a group of Hungarian scientists, who have speculated that the objects are actually colonies of photosynthetic Martian microorganisms that emerge each year to sunbathe in the warm weather.

Tuesday 2 October 2012

SIMU ZAIDI YA MILION 1 ZA KICHINA ZAZIMWA

Kwa mara ya kwanza jana zaidi ya simu milioni moja za bandia nchini ziligeuka ‘makopo’ baada ya kuzimwa na tume ya mawasiliano  nchini, CCK.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa CCK Francis Wangusi alisema Airtel imeziondolea mawasiliano simu 740,000, Safaricom 680,000, wakati mtandao wa Orange ukizipiga chini simu 75,000.
Pia serikali imesema ina mpango wa kuondoa kodi kwenye simu ili kuzifanya simu halali ziweze kuwa na bei nafuu ambazo wananchi wa Kenya watazimudu.
 CCK imesema idadi ya simu bandia inaweza kuwa chini ya milioni 2.5 tofauti na ilivyokuwa imekadiria mwanzo na kuongeza kuwa wananchi wengi nchini walikuwa wameshanunua simu halali.
“Wale ambao simu zao bado zinafanya kazi na ni bandia wasisherehekee kwasababu nazo zitazimwa na ni kwa maslahi ya nchi hii,” alisema Wangusi.

Monday 1 October 2012

Hatari ya Al-shaabab Nchini

Shambulio laua mtoto na kujeruhi wengine kanisani

Mtoto mmoja aliuawa papo hapo na wengine zaidi ya 10 wakajeruhiwa kwenye shambulio la guruneti katika Kanisa la St Polycarp ACK, barabara ya Juja, Mtaa wa Eastleigh, Nairobi, Jumapili.

Afisa mmoja wa matibabu katika hospitali ya Radiant, eneo la Mlango Kubwa, alisema mtoto huyo mvulana kwa jina Ian Mario Maina, aliyetimu umri wa miaka tisa Jumamosi, alipelekwa hospitalini akiwa tayari ameaga dunia.


“Alikuwa na majeraha mabaya mikononi, sehemu za tumbo na miguuni,” akasema afisa huyo, na kuomba tusimtaje jina kwa sababu hana ruhusa kuzungumza kwa niaba ya hospitali hiyo.

Biwi la simanzi lilitanda katika hospitali hiyo, huku marafiki wakimliwaza mama ya mtoto huyo, ambaye alilemewa na majonzi kwa kumpoteza mwanawe ghafla.

Watoto wanne waliokuwa na majeraha madogo miguuni na kichwani, na mwanamke aliyepatwa na mshtuko, walipelekwa Guru Nanak, huku saba waliojeruhiwa vibaya wakipelekwa katika hospitali ya Radiant iliyo karibu na kanisa hilo, kabla ya kuhamishwa hadi Kenyatta.

Mkuu wa Polisi eneo la Starehe, Bw Samuel Anampiu, wavamizi katika shambulio hilo lililotokea mwendo wa saa 4.30 asubuhi walitumia bomu la kujitengenezea.

“Maafisa wetu wamekusanya vipande ambavyo vitafanyiwa uchunguzi wa kina,” akasema.

Kujibizana

Iliripotiwa kuwa awali wanaume wawili walionekana wakijibizana na walinzi wa kanisa hilo kabla ya kuondoka kwa miguu.

Muumini mmoja wa kanisa hilo, Bi Anne Wanjiru Murage, alisema alisikia mlipuko kisha waumini wakaanza kutawanyika wakielekea mahali kunapokuwa na ibada ya watoto.

“Tuliskia mlipuko mkubwa kisha tukaona vumbi katika jengo ambamo watoto huwa na ibada yao,” akasema Bi Murage, ambaye alipeleka watoto wanne, akiwemo mwanawe, katika hospitali ya Guru Nanak.

Alisema bomu hilo lilitupwa kutoka nje ya kanisa, na kuanguka ndani ya darasa linalotumiwa kwa ibada ya watoto. “Kuna ua ambalo limezunguka kanisa na pia kuna askari wanaokagua kila mtu anayeingia kanisani. Bomu hilo lilirushwa kutoka upande wa nyuma, ambapo kanisa limepakana na maeneo ya makazi,” akasema.

Hali ya taharuki ilitanda katika eneo hilo baada ya wakazi wanaoaminika kuwa Wakristo kutishia kuwatimua wenzao wa Kiislamu.

Vijana hao waliojiunga kwa makundi walishambulia mijengo kadha kwa mawe na kutishia kuichoma moto.

Maafisa wa GSU waliungana na polisi wa kawaida katika kupiga doria mchana mzima ili kudumisha utulivu.

Mbunge wa Starehe, Bi Margaret Wanjiru, alitembelea eneo hilo na kukashifu kitendo hicho, huku akitaka Serikali ichunguze kwa kina kiini na wahusika wa shambulio hilo.

Washukiwa

Polisi walikamata watu wanne, ambao walijitambulisha kuwa wanahabari wa shirika la Horn Cable TV.

Kisa hicho kilitokea siku mbili tu baada ya wanajeshi wa KDF, wakishirikiana na wale wa Muungano wa Afrika (Amisom), kuwatimua wanamgambo wa Al-Shabaab kutoka ngome yao ya Kismayu, Somalia. Al-Shabaab wameapa kulipiza kisasi.

Kitengo cha habari cha Harakat Al-Shabaab Al Mujahideen, vuguvugu la utawala wa Kusini na Kati mwa Somalia, linaloshirikiana na Al-Shabaab, lilitangaza baadaye kuwa KDF ilidhihirisha vita vyao vilikuwa dhidi ya dini ya Kiislamu.

Kupitia mtandao wa 'Twitter’, utawala huo ulilaumu KDF kwa kuendeleza mashambulizi Kismayu licha ya kuwa wanamgambo walikuwa wameondoka.

Walidai kuwa watoto wawili walifariki katika mashambulizi yaliyofanywa usiku wa kuamkia jana.



Maswala ya mashambulizi kutoka kwa kundi la Al-shabaabyanazidi kuongezeka huku Wanajeshi wetu wakipabana na kundi hili kule Somalia tukio hili linasemekana nikama majibu Kundi hili kwa Nchini hii baada ya KDF kuteka mji wa Kisimayu.